Simba Day 2026 kufanyika Uwanja wa Uhuru Agosti 8

Jul 22, 2026 - 16:15
0 0
Simba Day 2026 kufanyika Uwanja wa Uhuru Agosti 8

By  Mwandishi Wetu

Mwananchi Communications Limited

Klabu ya Simba imetangaza kuwa kilele cha tamasha la Simba Day 2026 kitafanyika Agosti 8, 2026 katika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam, huku kikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 90 tangu kuanzishwa kwa klabu hiyo.

Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally, amesema hayo leo Jumatano Julai 22, 2026 wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, ambapo amesema awali walikuwa na matarajio ya kufanyia tamasha hilo katika Uwanja wa Benjamin Mkapa kutokana na ukubwa wa tukio hilo, lakini uwanja huo upo kwenye matengenezo.

“Simba Day 2026 itafanyika kwenye Uwanja wa Uhuru. Kutokana na ukubwa wa tamasha hili duniani tunatamani kufanyika kwenye Uwanja wa Mkapa, lakini kwa sasa upo kwenye matengenezo hivyo uwanja ambao utatumika ni Uwanja wa Uhuru,” amesema Ahmed.

Ameongeza kuwa tamasha hilo litakuwa la kipekee kwa kuwa litakwenda sambamba na kumbukumbu ya miaka 90 ya Simba Sports Club, huku mashabiki wakitarajiwa kushiriki katika matukio mbalimbali ya kuadhimisha historia ya klabu hiyo.

Comments (0)

User
🔒
SALAMA NA RAHISI KUJIUNGA

JIUNGE NA SOGA COMMUNITY

MASHABIKI WA MICHEZO NA MATUKIO DUNIANI WANAKUTANA HAPA. HAKUNA FUJO, HAKUNA MATUSI — NI MAZUNGUMZO YA MAANA NA MARAFIKI WAPYA.

✅ HAKUNA MADHARA KUJIUNGA NA CHAT YETU
✅ MFUMO UNAZUIA CHATS ZISIZOFAA
✅ KUBLOCK USER ASIYE NA MAADILI
✅ KUMSHITAKI NA KUMFUKUZA MTUMIAJI MBAYA
✅ KUFOLLOW NA KUBEFRIEND WATUMIAJI WENYE MAADILI

What's Your Reaction?

Like Like 0
Dislike Dislike 0
Love Love 0
Funny Funny 0
Wow Wow 0
Sad Sad 0
Angry Angry 0