Heche adai viongozi 51 wa CHADEMA wamekamatwa, awataka mawakili kujiandaa

Aug 15, 2026 - 04:15
0 0
Heche adai viongozi 51 wa CHADEMA wamekamatwa, awataka mawakili kujiandaa

Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, John Heche, amedai kuwa jumla ya viongozi 51 wa chama hicho wamekamatwa katika kanda mbalimbali nchini na baadhi yao wanakabiliwa na mashtaka ya uhaini.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza leo Julai 25, 2026, Heche amesema kati ya waliokamatwa, viongozi 23 wanatoka Kanda ya Victoria, 17 Kanda ya Serengeti na 11 Kanda ya Nyasa.

“Viongozi wa CHADEMA kwa Kanda tatu, Kanda ya Victoria wamekamatwa watu 23, Kanda ya Serengeti watu 17 na Kanda ya Nyasa watu 11, jumla kuna viongozi wa CHADEMA 51 wamekamatwa na kubambikizwa kesi kubwa ya uhaini, hapo ni mbali na mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma,” alisema Heche.

Katika mkutano huo, Heche aliwataka mawakili wa chama hicho kujiandaa kuwapa msaada wa kisheria viongozi wanaoshikiliwa, akisisitiza kuwa CHADEMA itatumia njia zote za kisheria kuhakikisha wanaachiliwa.

“Hata makande tutakula ili watoke,” alisema.

Mamlaka za serikali hazikuwa zimetoa tamko kuhusu madai ya kukamatwa kwa viongozi 51 wa CHADEMA au tuhuma za kubambikiziwa kesi kufikia wakati wa kuchapishwa kwa taarifa hii.

Kauli za Heche zinaakisi msimamo wa chama hicho na madai hayo hayajathibitishwa na upande wa serikali.

Comments (0)

User
🔒
SALAMA NA RAHISI KUJIUNGA

JIUNGE NA SOGA COMMUNITY

MASHABIKI WA MICHEZO NA MATUKIO DUNIANI WANAKUTANA HAPA. HAKUNA FUJO, HAKUNA MATUSI — NI MAZUNGUMZO YA MAANA NA MARAFIKI WAPYA.

✅ HAKUNA MADHARA KUJIUNGA NA CHAT YETU
✅ MFUMO UNAZUIA CHATS ZISIZOFAA
✅ KUBLOCK USER ASIYE NA MAADILI
✅ KUMSHITAKI NA KUMFUKUZA MTUMIAJI MBAYA
✅ KUFOLLOW NA KUBEFRIEND WATUMIAJI WENYE MAADILI

What's Your Reaction?

Like Like 0
Dislike Dislike 0
Love Love 0
Funny Funny 0
Wow Wow 0
Sad Sad 0
Angry Angry 0