August 27, 2026

UFARANSA: Kwa upande wa soka la vilabu, macho sasa yanaelekezwa kwenye msimu mpya wa Champions League baada ya kumalizika kwa Kombe la Dunia lililofanyika Amerika Kaskazini.

Ligi kubwa barani Ulaya zimeanza kurejea katika ratiba yake, huku vilabu vikubwa vikisubiri kufahamu wapinzani wao katika hatua ya ligi ya Champions League kupitia droo inayofanyika Alhamisi.

Paris Saint-Germain (PSG) itaanza kampeni yake ikiwa na lengo la kutwaa taji hilo kwa mara ya tatu mfululizo.

PSG ilitwaa ubingwa wa Ulaya msimu uliopita baada ya kuifunga Arsenal kwa mikwaju ya penalti katika fainali iliyochezwa Budapest.

Ikiwa PSG itafanikiwa kutwaa tena taji hilo, itaweka historia ya kipekee, kwani Real Madrid ya mwaka 2016 hadi 2018 ndiyo timu pekee katika kipindi cha miaka 50 iliyopita iliyofanikiwa kuwa mabingwa wa Ulaya kwa misimu mitatu mfululizo.

The post PSG kusaka historia ya makombe matatu mfululizo first appeared on SpotiLEO.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *