Rais Samia Apongeza Hatua ya Maridhiano ya Kisiasa Zanzibar (Picha +Video)

Jul 09, 2026 - 13:15
0 0
Rais Samia Apongeza Hatua ya Maridhiano ya Kisiasa Zanzibar (Picha +Video)

Global Publishers July 9, 2026 0 views 0 Comments

SHARE THIS:

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema uungwana haupaswi kuzaa kiburi wala kutoweka nafasi ya kusikilizana, akisisitiza kuwa matarajio makubwa ya wananchi ni kuona nchi ikiendelea kuwa na amani, utulivu na mshikamano.

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo alipohudhuria hafla ya kushuhudia utiaji saini wa Tamko la Pamoja la Maridhiano ya Kisiasa kati ya vyama vya siasa Zanzibar, iliyofanyika katika Ikulu ya Zanzibar.

Amesema maridhiano, mazungumzo na kuheshimiana ni msingi muhimu wa kujenga taifa lenye umoja na maendeleo, huku akisisitiza kuwa viongozi wanapaswa kuweka mbele maslahi ya wananchi badala ya tofauti zao za kisiasa.

Kauli ya Rais Samia imekuja katika hafla inayotajwa kuwa hatua muhimu ya kuimarisha maelewano ya kisiasa na kudumisha amani nchini, hususan Zanzibar.


SHARE THIS:

Comments (0)

User
🔒
SALAMA NA RAHISI KUJIUNGA

JIUNGE NA SOGA COMMUNITY

MASHABIKI WA MICHEZO NA MATUKIO DUNIANI WANAKUTANA HAPA. HAKUNA FUJO, HAKUNA MATUSI — NI MAZUNGUMZO YA MAANA NA MARAFIKI WAPYA.

✅ HAKUNA MADHARA KUJIUNGA NA CHAT YETU
✅ MFUMO UNAZUIA CHATS ZISIZOFAA
✅ KUBLOCK USER ASIYE NA MAADILI
✅ KUMSHITAKI NA KUMFUKUZA MTUMIAJI MBAYA
✅ KUFOLLOW NA KUBEFRIEND WATUMIAJI WENYE MAADILI

What's Your Reaction?

Like Like 0
Dislike Dislike 0
Love Love 0
Funny Funny 0
Wow Wow 0
Sad Sad 0
Angry Angry 0